SULEIMAN MAGOGOMA BLOG PROMO

BREAKING NEWS:MACHAFUKO MTWARA, OFISI YA CCM YACHOMWA H344

Hali ilivyo Mtwara kwa sasa, barabara zimefungwa, mabomu ya machozi na matairi yakichomwa moto.

MTWARA SI SHWARI WAKATI HUU.
MAPAMBANO kati ya Askari wa Jeshi la Polisi na Wananchi wa Mkoa wa Mtwara umefika katika hatua mbaya,kiasi cha mtu mmoja kudaiwa kujeruhiwa vibaya baada ya kurushiwa bomu wakati wa mashambulizi hayo katika eneo la Magomeni.

Mbali na kujeruhiwa kwa mtu huyo aliyekuwa katika maandamano ya kupinga Bajeti ya Wizar
a ya Nishati na Madini, Ofisi ya Chama Cha  Mapinduzi (CCM) pia imechomwa moto.

Taarifa zilizopo hivi punde zinadai kwamba wananchi wa Mkoa wa Mtwara wamefungiwa majumbani tangu asubuhi, huku
Jeshi la Polisi likifanya msako wa nyumba hadi nyumba kwa lengo la kuwanasa watuhumiwa wanaodaiwa kuchochea maandamano hayo kwa njia ya vipeperushi.


Shuhuda wa wa tukio hilo ameeleza kuwa waandamanaji hao wameapa kufa endepo serikali itaendelea na mipango yake ya kusafirisha gesi hiyo hadi Jijini Dar es Salaam.  

"Hali hapa ni mbaya, tangu asubuhi wananchi wote wamefungiwa ndani ya majumba yao, hakuna anayeruhusiwa kutoka nje,Polisi wanapiga  mabomu ya machozi kila mtaa huku wakiwasaka watuhumiwa waliosambaza vipeperushi na kuwatawanya wandamanaji waliozagaa katika mitaa  mbalimbali, mpaka hivi sasa kuna mtu mmoja ameripotiwa kujeruhiwa vibaya katika mashambulizi ya raia na Asakari Polisi wanaotumia mabomu ya machozi na silaha zigine za moto"alisema shuhuda wa tukio hilo.

Hata hivyo imedaiwa kuwa hali hiyo imesababisha barabara zote kufungwa kiasi cha kuzuia mabasi yanayoingia na kutoka katika mji huo toka asubuhi, kuna baadhi ya mitaa matairi yamechomwa moto barabarani, magari ya FFU yametanda kila kona za mji, huku taarifa zidi ikifafanua kwamba hakuna mawasiliano, milio ya mabomu inasikika kila kona na hali ya utulivu sio ya kuridhisha, Askari wa zima moto wamesambaa kuzima moto na kuna baadhi ya nyumba maeneno ya Shangani zimechoma moto. 
Chanzao http://www.habarimpya.com
TUPE MAONI YAKO

TAARIFA KUHUSU MATANGAZO YA KAZI SERIKALINI

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira, Bw. Xavier Daudi akifafanua jambo. Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Sekretarieti ya Ajira, Bw. Bakari Mahiza.
Waombaji waliotuma maombi ya fursa za ajira kwa ajili ya matangazo yaliyokuwa yametolewa na Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma  kwa niaba ya Waajiri mbalimbali nchini mnamo  tarehe 26 Machi, 2013 moja likiwa katika lugha ya Kiingereza na lingine katika lugha ya Kiswahili ambapo mwisho wa kutuma maombi ilikuwa tarehe 9 Aprili, 2013 wametakiwa kutembelea tovuti ya Sekretarieti ya Ajira mara kwa mara ili kupata ratiba ya usaili kwa nafasi walizoomba.
Katibu wa Sekretarieti ya Ajira Bw. Xavier Daudi amesema  hayo leo alipokuwa akiongea na baadhi ya wadau waliomtembelea ofisini kwake wakitaka ufafanuzi wa masuala mbalimbali yanayohusu mchakato wa Ajira Serikalini.
Amesema ofisi yake itaendelea kuwafahamisha wale wote walioomba  nafasi za kazi Serikalini kadri siku zinavyosogea. Amebainisha kuwa kwa tangazo la kiingereza lililotolewa tarehe 26 Machi, 2013 ambalo lilihusu Taasisi za Umma  zaidi, usaili wake utaanza tarehe 20 mwezi huu kama ratiba ilivyoainisha katika tangazo la kuwaita kwenye usaili lililotolewa tahere 16 Mei, 2013 kupitia tovuti ya Sekretarieti ya Ajira likibainisha usaili utafanyika tarehe ngapi na sehemu gani pamoja na orodha ya majina ya wahusika waliokidhi vigezo vya tangazo kwa  nafasi hizo.
Daudi  amewataka waombaji wa tangazo lililokuwa limetolewa kwa lugha ya Kiswahili tarehe tarehe 26 Machi, 2013 waendelee  kuvuta subira kwani ratiba yake ya Usaili kwa waombaji wenye Sifa itatolewa mara baada ya Usaili wa Tangazo la Kingereza kukamilika ili kuepuka kuwachanganya waombaji. Pamoja na hayo amewataka waombaji hao kukaa tayari kwani usaili wa tangazo hilo unaweza kufanyika wakati wowote mwezi Juni mwaka huu ila tarehe rasmi na wapi watajulishwa baadae.
Aidha, Waombaji wa nafasi wazi za kazi  kwa tangazo la kazi lililotolewa kupitia tovuti hii tarehe  16 Aprili, 2013 ambalo mwisho wake wa kutuma maombi ilikuwa tarehe 2 Mei, 2013,  wanafahamishwa kuwa mchakato wa kuchambua maombi yao bado unaendelea na watapewa taarifa ya kuitwa kwenye usaili kwa wale waliokidhi vigezo vya tangazo mara baada ya taratibu zote kukamilika.
Katibu huyo pia ametoa Rai kwa waombaji wote waliochaguliwa kuja kufanya usaili kujiandaa vyema ikiwa ni pamoja na kuzingatia vitu muhimu wanavyopaswa kuja navyo kwenye usaili ikiwemo vyeti vya Kitaaluma.
Daudi alimalizia kwa  kuwatahadharisha waombaji wa fursa za Ajira serikalini pamoja na wadau  kuwa makini na baadhi ya Matangazo ya Ajira ambayo yanatolewa kupitia baadhi ya mitandao ya kijamii hususani wa  www.eastafricajobscareer.com yenye lengo la kupotosha jamii. Ofisi yake imefikia hatua ya kusema haya kutokana na mtandao huo alioutaja hapo juu kuchukua matangazo ya taasisi yake na kuyabadilisha tarehe za kutolewa, mwisho wa kutuma maombi, kumbukumbu namba pamoja na vichwa vya habari na kuyaweka hewani ilihali wakijua wazi hayajatolewa na Sekretarieti ya Ajira.

Hivyo amewataka wadau wote kuyapuuza matangazo hayo ya uongo yenye nia ya kuwapotosha. Aidha, amewahimiza wananchi pindi wanapoona matangazo ya kazi yanayoihusisha Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma katika mitandao au mbao za matangazo kujiridhisha ili kuyathibitisha kupitia  tovuti ya www.ajira.go.tz ili kuwa na uhakika zaidi kuliko kudanganywa na kutuma barua za maombi kwa matangazo ambayo si ya kweli.
Imetolewa na  Kitengo cha Mawasiliano Serikalini.
Ofisi ya Rais-Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
Kwa maelezo zaidi; wasiliana na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Kwa barua pepe;  gcu@ajira.go.tz au simu 255-687624975
20 Mei, 2013
TUPE MAONI YAKO

MAVETERAN WA BAPA NA PSPA-UDOM. HAMNA MBABE WACHOSHANA NGUVU KWA MABAO 1-1. SHANGWE ZILIZOKUWEPO UWANJANI NI BALAA IT WAZ MORE THAN CRAZY. JIACHIE NA CAMERA YA SULE THE BLOGGER KWA KU PREMER EVENT NZIMA

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 

  
Flowers  na washkaji wa bapa na pspa katika pozi
 
 
 
 
 
Tuli enjoy kinomanoma ilikuwa ni bonge moja  la game.  It waz History in the making. bapa na pspa ni ndugu 4rever
TUPE MAONI YAKO

MAGAZETI YA LEO ALHAHISI MAY 16 HAYA HAPA

DSC 0198 b6684
DSC 0199 c9faa
DSC 0200 7985f

DSC 0202 1be70
DSC 0203 33ab2
DSC 0204 a095b
DSC 0205 15543
DSC 0206 6a929
DSC 0207 fba28
DSC 0208 12c22
DSC 0209 fa0ba
DSC 0210 ca5d9
DSC 0211 b7e8a
DSC 0212 df6f9
DSC 0213 2d894DSC 0214 e2944
TUPE MAONI YAKO

Nyuki wafukuza Tembo Rombo

tembo 02 e84d4
HALMASHAURI ya Wilaya ya Rombo imeanza mipango ya kutumia ufugaji wa nyuki kukabiliana na tembo waharibifu ambao mara kadhaa huvamia baadhi ya makazi ya wananchi maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo na kufanya uharibifu wa mazao pamoja na kuua au kujeruhi wakazi
.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi hivi karibuni wilayani hapa, Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo, Judethadeus Mboya alisema tayari halmashauri hiyo imetengeneza mizinga ya nyuki ambayo imesambazwa maeneo kadhaa ili kukabiliana na tembo waharibifu eneo hilo.
"Unajua nimetembea mbuga mbili za Kenya ikiwemo Tsavo ambazo tumepakana nazo eneo hili sehemu ambayo tembo hutokea huko na kuvamia maeneo yetu, sehemu hizi wao wamedhibiti uvamizi wa tembo...wamefuga nyuki wengi sana na maeneo mengine wametumia hadi teknolojia kuwazuia tembo kuvamia makazi ya raia hivyo hawapati madhara kama yetu," alisema Mboya akifanya mazungumzo na gazeti hili ofisini.
Alisema kwa sasa tayari wametengeneza mizinga 50 ya nyuki na kuifunga ukanda wa chini wa vijiji kama Chala, Ibukoni, Ngoyoni na maeneo mengine ambayo tembo huyatumia kama njia kipindi cha uvamizi na kwa sasa mizinga mingine 100 ya nyuki inaandaliwa kuenezwa maeneo mengine kukabiliana na tembo hao hatari.
Alisema viongozi wa halmashauri hiyo pia wametoa elimu kwa wanakijiji maeneo husika ya kuhamasisha uvugaji nyuki katika vikundi ikiwa ni jitihada za kukabiliana na tembo hao waharibifu ambao idadi kubwa hutokea nchi jirani ya Kenya na kufanya uharibifu pamoja na kutishia maisha ya wanavijiji upande wa Tanzania.
Aidha kiongozi huyo alisema tembo hao mbali na kufanya uhalibifu mkubwa wa mazao ya wanavijijini kipindi cha uvamizi wakati mwingine wamekuwa wakiuwa raia jambo ambalo ni hatari zaidi kiusalama.
Uchunguzi uliofanywa na mwandishi umebaini uvamizi wa wanyama hao umekuwa kero kwa maeneo mbalimbali ya vijiji vya wilaya hiyo, kiasi ambacho unatishia shughuli za maendeleo ya wananchi kama kilimo pamoja na maendeleo ya elimu kwa ujumla.
Akizungumzia hali ya uvamizi wa tembo na athari za elimu, Mwalimu wa Taaluma Shule ya Sekondari Tanya, Shuma Himidiel alisema miezi ambayo tembo huanza kufanya uvamizi huingilia ratiba za masomo na mara kadhaa kusimama kutokana na hofu ya wanafunzi na usalama wao hasa wanapotoka na kuja shuleni.
"Kimsingi wanyama hawa wanapoanza usumbufu kijiji kizima huwa na heka heka na wakati mwingine hata wanafunzi wanashindwa kuja shule kuhofia maisha yao...hata wazazi huwazuia watoto wao kutoka hadi hali ya hatari inaporejea kuwa ya kawaida.
Akifafanua zaidi mwalimu Himidiel alisema mara ya mwisho tembo kufanya uvamizi katika Kijiji cha Tanya waliua mtu mmoja walipokuwa wakidhibitiwa na askari wa wanyamapori eneo hil
SLUT KWA MJENGWA BLOG
TUPE MAONI YAKO

MAGAZETI YA LEO JUMATANO MAY 15 HAYA HAPA.

DSC 0001 aebb0
DSC 0002 30fba
DSC 0003 9d5d6
DSC 0004 cb311
DSC 0005 14caf

DSC 0006 e193d
DSC 0007 1d3a2
DSC 0008 236cc
DSC 0009 48c8b
DSC 0010 e3a3f
DSC 0011 a012b
DSC 0012 cc4c4
DSC 0013 aadc3
TUPE MAONI YAKO
 

SULEIMAN MAGOMA Copyright © 2011 -- Template created by Suleiman Magoma -- Powered by Magoma Co.LTD